• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Kasulu Town Council
Kasulu Town Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Kasulu Town Council

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Strategies
  • Administration
    • Organisation Structure
    • Department
      • ELIMU SEKONDARI
      • ELIMU AWALI NA MSINGI
        • MAENDELEO YA JAMII
      • MAENDELEO YA JAMII
      • MIUNDOMBINU MAENDELEO YA MJINI NA VIJIJINI
      • HUDUMA ZA AFYA USTAWI WA JAMII NA LISHE
      • VIWANDA BIASHARA NA UWEKEZAJI
      • KILIMO MIFUGO NA UVUVI
      • MIPANGO NA URATIBU
      • UTAWALA NA USIMAMIZI WA RASILIMALI WATU
    • Units
      • USIMAMIZI WA TAKA NGUMU NA USAFI WA MAZINGIRA
      • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
      • FEDHA NA UHASIBU
      • HUDUMA ZA SHERIA
      • UKAGUZI WA NDANI
      • USIMAMIZI WA UNUNUZI
      • TEHAMA
      • MAWASILIANO SERIKALINI
      • NMALIASILI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
      • MALIASILI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
  • Investment opportunities
    • Agriculture
    • Livestock
  • Our Services
    • Health
    • Education
    • Agriculture
  • Councillors
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Ratiba
      • Ratiba
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipango Miji Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Uchumi Elimu Afya na Maji
  • Projects
    • Proposed Projects
    • On-going-Projects
    • Completed Projects
  • Publications
    • Brochures
    • By Law
    • Strategic Plan
    • Reports
  • Media Centre
    • Video
    • Press Release
    • Speeches
    • Photo Gallery

BOOST YABORESHA ELIMU YA AWALI KASULU

Posted on: May 16th, 2025

Kasulu, Tanzania

Serikali kupitia Mradi wa BOOST imepiga hatua kubwa katika kuboresha elimu ya awali nchini, kwa kuimarisha mazingira ya ujifunzaji na ufundishaji, pamoja na miundombinu na upatikanaji wa zana za kufundishia.

Akizungumza baada ya kukamilika kwa zoezi la ufuatiliaji lililohusisha Maafisa wa Uthibiti Ubora wa Elimu kutoka Halmashauri ya Mji Kasulu pamoja na Ofisi ya Mawasiliano Serikalini, Afisa Elimu ya Awali na Msingi Bw. Julius Buberwa alisema kila shule ya msingi sasa ina darasa la elimu ya awali, hivyo kila mwanafunzi anayeanza shule ya msingi anakuwa tayari amepitia msingi huo muhimu wa awali.

Katika juhudi hizo, serikali kupitia mradi huo imefanikiwa kujenga madarasa ya mfano katika shule tano za Murusi, Bajana, Juhudi, Kidyama na Mumnyika. Buberwa alisema madarasa hayo yameleta mabadiliko makubwa kwa kuongeza mvuto wa elimu ya awali na kusababisha ongezeko la wanafunzi wanaoandikishwa katika shule za serikali ikilinganishwa na miaka ya nyuma.

“Madarasa haya si tu yameboresha mazingira ya ujifunzaji, bali pia yameongeza hamasa kwa wazazi kupeleka watoto wao shule,” alisema Buberwa.

Pamoja na ujenzi wa miundombinu, walimu wa madarasa ya awali wamepewa mafunzo mahsusi juu ya mbinu bora za kufundisha na namna ya kutumia zana za kufundishia. Mafunzo hayo yameleta maboresho makubwa darasani kwa kuifanya elimu ya awali kuwa ya kuvutia na rahisi kueleweka kwa watoto. Katika kuimarisha matumizi ya zana hizo, serikali kupitia Halmashauri ya Mji Kasulu imepeleka fedha kwa ajili ya utengenezaji wa zana za kufundishia kwa shule mbalimbali.

Katika kipindi cha awamu ya kwanza, shule 10 zilipokea kiasi cha Shilingi 585,500/= kila moja, na kwa awamu ya pili, shule 29 zimepokea Shilingi 675,000/= kila moja. Bw. Buberwa alitumia nafasi hiyo kuishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuleta mageuzi chanya katika sekta ya elimu. “Shule za serikali sasa zinaonekana bora, na tofauti kati ya shule za umma na binafsi inaendelea kupungua,” aliongeza.

Mradi wa BOOST umeendelea kuwa chachu ya maendeleo ya elimu ya awali nchini kwa kuhakikisha kuwa watoto wanapata fursa sawa ya kuanza elimu katika mazingira salama, rafiki, na yaliyoandaliwa kitaalamu.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Kasulu Mwl Vumilia J. Simbeye amemshukuru kwa dhati Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kuboresha miundombinu ya Sekta ya Elimu Msingi na Sekondari Nchini Tanzania kupitia Miradi mbalimbali ya kimkakati ikiwemo ile ya BOOST na SEQUIP.

____________________________________

Announcements

  • NAFASI ZA KAZI March 19, 2025
  • TANGAZO LA UBORESHAJI DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA April 30, 2025
  • View All

Latest News

  • Mkurugenzi Simbeye Aamsha Ari Mpya Kasulu Mji: Aanzisha Timu za Michezo kwa Watumishi, Aweka Historia Mpya ya Ushirikiano Kazini.

    May 17, 2025
  • BOOST YABORESHA ELIMU YA AWALI KASULU

    May 16, 2025
  • KAIMU KATIBU TAWALA MKOA NDUGU ELIASANTE M.MBOELO AKABIDHIWA VIFAA TIBA HUDUMA ZA MACHO MKOANI KIGOMA

    May 08, 2025
  • KAIMU KATIBU TAWALA MKOA NDUGU ELIASANTE M.MBOELO AKABIDHIWA VIFAA TIBA HUDUMA ZA MACHO MKOANI KIGOMA

    May 08, 2025
  • View All

Video

UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA
More Videos

Quick Links

  • News

Related Links

  • TAMISEMI
  • Ega
  • Utumishi
  • Kigoma Region

World visitors tracker

world map hits counter

Contact Us

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service
    • Test

Copyright ©2017 Kasulu Town Council. All rights reserved.