• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Kasulu Town Council
Kasulu Town Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Kasulu Town Council

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Strategies
  • Administration
    • Organisation Structure
    • Department
      • ELIMU SEKONDARI
      • ELIMU AWALI NA MSINGI
        • MAENDELEO YA JAMII
      • MAENDELEO YA JAMII
      • MIUNDOMBINU MAENDELEO YA MJINI NA VIJIJINI
      • HUDUMA ZA AFYA USTAWI WA JAMII NA LISHE
      • VIWANDA BIASHARA NA UWEKEZAJI
      • KILIMO MIFUGO NA UVUVI
      • MIPANGO NA URATIBU
      • UTAWALA NA USIMAMIZI WA RASILIMALI WATU
    • Units
      • USIMAMIZI WA TAKA NGUMU NA USAFI WA MAZINGIRA
      • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
      • FEDHA NA UHASIBU
      • HUDUMA ZA SHERIA
      • UKAGUZI WA NDANI
      • USIMAMIZI WA UNUNUZI
      • TEHAMA
      • MAWASILIANO SERIKALINI
      • NMALIASILI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
      • MALIASILI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
  • Investment opportunities
    • Agriculture
    • Livestock
  • Our Services
    • Health
    • Education
    • Agriculture
  • Councillors
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Ratiba
      • Ratiba
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipango Miji Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Uchumi Elimu Afya na Maji
  • Projects
    • Proposed Projects
    • On-going-Projects
    • Completed Projects
  • Publications
    • Brochures
    • By Law
    • Strategic Plan
    • Reports
  • Media Centre
    • Video
    • Press Release
    • Speeches
    • Photo Gallery

DAS MTEWELE AIASA JAMII KUWALINDA NA KUWATHAMINI WAZEE NA WATU WENYE ULEMAVU

Posted on: February 21st, 2025

Ameyaeleza hayo leo wakati akifungua rasmi kikao cha wajumbe wa  balaza la wazee na watu wenye ulemavu Halmashauri ya Mji Kasulu kilichofanyika katika ukumbi wa halmashauri na kuwahusisha viongozi mbalimbali wa wa vyama vya walemavu na wawakilishi wa wazee.

Katika kikao hicho kilichoratibiwa na Halmashauri ya Mji kwa ufadhiri wa Shirika lisilo la kiserikali HelpAge Tanzania Katibu tawala Bi Teresia Mtewele ameonya tabia ya baadhi ya wazazi kutowapa thamani sawa watoto wenye ulemavu na kuwatenga au kuwaficha kwa kuona kama laana kuzaa watoto wenye hali hizo.

 Mtewele amesema  Serikali imeweka mipango Madhubuti ya kudhibiti vitendo vya ukatili kwa watu kutoka makundi maalum na kutenga fedha kwa ajili ya kusaidia makundi haya katika Nyanja mbalimbali ikiwemo afya Pamoja na elimu.

Aidha Katibu tawala huyo ameionya tabia ya baadhi ya wazazi kuwafanya watoto wenye ulemavu kitega Uchumi na kuwatembeza huku na kule wakiomba msaada badala yake wawasaidie kwa kuwawezesha kupata haki zao za msingi kwani wanaweza kutimiza ndoto zao kama watoto wengine

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Shirikisho la Vyama Vya Walemavu Kasulu Zakayo Nkohozi

ameishukuru serikali kwa namna inavyoendelea kuwakumbuka na  kuwashirikisha watu wenye mahitaji maalum katika shughuli mbalimbali na kuwapatia msaada mbalimbali kutatua changamoto wanazopitia ikiwemo kuwapatia vifaa wezeshi. Aidha amesema huko nyuma walemavu walipuuzwa na kuonekana hawana uwezo wa kufanya chochote lakini serikali inaendelea kuwapa mafunzo yanayowawezesha kujitambua na kujihusisha katika shughuli mbalimbali za kiuchumi zinazowawezesha kupata kipato na hivyo kujikimu kimaisha badala ya kuomba omba mitaani.

Kwa upande wake Afisa Ustawi Wa jamii Ndugu Festo Pansian Solly amesema kumekuwepo na changamoto ya makundi ya wazee na watu wenye ulemavu kutokujua sera, miongozo na sheria zinazo wahusu na kuongeza kwamba  wazee na watu wenye ulemavu haya ni makundi yanayoshabihiana hasa kwenye changamoto zao  na hivyo yanahitaji uangalizi wa kipekee hivyo,halmashauri kwa kulijua hili imeona ni vyema kuyakutanisha makundi haya na kuwapitisha katika kuwaelekeza majukumu yao Pamoja na kuweka mpango mkakati wa namna ya kuhuisha mabalaza yatakayowawezesha kutatua changamoto zao.

Restituta Damiano mwakilishi kutoka Shirika la HelpAge Tanzania mkoa wa Kigoma ameishukuru Serikali kupitia Mkuu wa Wilaya ya Kasulu Pamoja na Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Mji Kasulu kwa namna wanavyowawezesha kufanya shughuli zao za kuwawezesha wazee na watu wenye ulemavu kujitegemea katika kufanya shughuli zao za kujikimu kimaisha na kuondokana na utegemezi unaopelekea kundi kubwa la ombaomba

Announcements

  • NAFASI ZA KAZI March 19, 2025
  • TANGAZO LA UBORESHAJI DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA April 30, 2025
  • View All

Latest News

  • KAIMU KATIBU TAWALA MKOA NDUGU ELIASANTE M.MBOELO AKABIDHIWA VIFAA TIBA HUDUMA ZA MACHO MKOANI KIGOMA

    May 08, 2025
  • KAIMU KATIBU TAWALA MKOA NDUGU ELIASANTE M.MBOELO AKABIDHIWA VIFAA TIBA HUDUMA ZA MACHO MKOANI KIGOMA

    May 08, 2025
  • KAIMU KATIBU TAWALA MKOA NDUGU ELIASANTE M.MBOELO AKABIDHIWA VIFAA TIBA HUDUMA ZA MACHO MKOANI KIGOMA

    May 08, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI KASULU TC LATOA PONGEZI

    May 05, 2025
  • View All

Video

UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA
More Videos

Quick Links

  • News

Related Links

  • TAMISEMI
  • Ega
  • Utumishi
  • Kigoma Region

World visitors tracker

world map hits counter

Contact Us

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service
    • Test

Copyright ©2017 Kasulu Town Council. All rights reserved.