Mkurugenzi wa Halmsahauri ya Mji kasulu Vumilia Julius Simbeye ameeongoza Jumuiya Akhlaqul Islam (JAI) kuchangia damu katika hospitali ya wilaya ya kasulu (Mlimani) ikiwa ni utaratibu wa jumuiya hiyo kujitolea damu ili kusaidia wenye uhitaji.
Tukio hilo lilofanyika leo Juni 8, ikihusisha takribani watu (150) wamechangia jumla ya unit (65) zimekusanya zikilenga kuwasaidia wagomjwa wenye uhitaji wakiwemo wajawazito, wagonjwa wa seli mundu, wagonjwa wa kansa ya damu, pamoja na majeruhi wa ajali.
Simbeye ameushukuru uongozi wa Jai kwa utaratibu wao wa kuhudumia hospitali hiyo kwa kuchangia damu lakini pia utaratibu wa kuhudumia wagonjwa wenye mahitaji na wale wasiokuwa na ndugu wa kuwahudumia pindi wanapolazwa pia ametoa rai kwa taasisi nyingine zikiwemo za dini na watu binafsi kuona umuhimu wa kuchangia damu.
Pia amewataka walio na mitazamo tofauti juu ya uchangiaji wa damu kuacha kwani utoaji wa damu ni kitendo salama na ina faida ikiwemo kupunguza magonjwa kama shinikizo la damu.
Aidha uongozi wa JAI umeeleza kuwa hii ni desturi waliojiwekea wakiwa wamelenga kupunguza vifo vinavyotokana na ukosefu wad amu ikiwepo mama wajawazito wanapotaka kujifungua na wale wanaopungukiwa na damu.
Ikumbukwe kuwa hii ni wiki ya uchangiaji damu duniani ikiwa na kauli mbiu "changia damu lete matumaini pamoja tunaokoa maisha."