• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Kasulu Town Council
Kasulu Town Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Kasulu Town Council

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Strategies
  • Administration
    • Organisation Structure
    • Department
    • Units
  • Investment opportunities
    • Agriculture
    • Livestock
  • Our Services
    • Health
    • Education
    • Agriculture
  • Councillors
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Ratiba
      • Ratiba
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipango Miji Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Uchumi Elimu Afya na Maji
  • Projects
    • Proposed Projects
    • On-going-Projects
    • Completed Projects
  • Publications
    • Brochures
    • By Law
    • Strategic Plan
    • Reports
  • Media Centre
    • Video
    • Press Release
    • Speeches
    • Photo Gallery

NAIBU WAZIRI TAMISEMI ASISITIZA URIPOTI KIDATO CHA KWANZA

Posted on: January 23rd, 2022

Naibu waziri wa Tamisemi Mh.David Silinde amethibitisha uwepo wa vyumba vya madarasa 57 vilivyokamilika pamoja na madawati ambavyo vinatumika kwa wanafunzi halmashauri ya mji wa kasulu na kupongeza halmashauri kwa kuweza kusimamia na kukamilisha madarasa hayo kwa wakati.

Ameyasema hayo januari 21 katika ziara ya ukaguzi aliyoifanya katika shule  17 halmashauri ya mji kasulu ambazo zilipata fedha kiasi cha shilingi bilioni 1,140,000,00 zilizotoka mfuko wa fedha wa  kimataifa (IMF) ikiwa ni fedha kwaajili ya mapambano dhidi ya ugonjwa wa uviko 19 na kusisitiza halmashauri kuhakikisha lile lengo ambalo mheshimiwa Rais SAMIA SULUHU HASSAN alilokusudia kuboresha na kujenga madarasa ya kisasa linatimia ikiwa ni pamoja na kuhimiza watoto wote waliochaguliwa kufika shuleni kupata elimu licha ya kukosa sare za shule kwa kuwa serikali iliruhusu mtoto kusoma bila ya kuwa na sare mpaka pale zitakapopatikana.

Aidha Silinde amemtaka mkuu wa wilaya ya kasulu Kanal Isaac Mwakisu kuhakikisha anapata takwimu sahihi ya kwanini idadi ya wanafunzi waliopo niwachache ukilinganisha na serikali iliyowachagua kujiunga na kidato cha kwanza kwa kuwahimiza wazazi kuwapeleka shule watoto wote waliochaguliwa.

Baadhi ya wanafunzi waliojiunga na kidato cha kwanza na wanatumia madarasa hayo wameishukuru serikali kupitia Mheshimiwa RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA SAMIA SULUHU  HASANI kwani uwepo wa madarasa hayo umesaidia kuongeza idadi ya shule mpya ambazo zitawasaidia watoto waliokuwa wakitumia umbali mrefu kufuata shule kuweza kupata ufaulu mzuri,kuwaepushia watoto wa kike kukumbana na ukatili wa kijinsia wa aina yoyote waliokuwa wakikutana nao wakati wakienda shuleni ambako walitumia umbali mrefu.

Kwaupande wake mkazi wa kijiji cha marumba kata ya Muhunga bw. Petro kalihadya amesema kuwa ujenzi wa shule hiyo mpya utakuwa umesaidia kwa wanafunzi kupunguza kutumia umbali wa km 25 kufuata shule katani muhunga ambapo ndipo kuna sekondari tegemezi inayohudumia  kata nzima yenye wakazi wengi na kugusia swala la serikali kuweka madarasa yenye viti na meza kutasaidia kuboresha elimu kwa watoto wao kutokana na familia nyingi hazikuwa na uwezo wa kupata vifaa hivyo na kuwataka watoto watakaoenda katika shule hiyo mpya inayotarajia kuanza muda wowote kusoma kwa bidii ili kuweza kufika juu Zaidi kielimu.  

Hata hivyo mkurugenzi wa halmashauri ya mji wa kasulu bw.Dollar Rajabu Kusenge amemshukuru Rais SAMIA SULUHU  HASSANI kwa kuweza kutoa pesa za ujenzi wa madarasa na shule mpya utaleta manufaa hasa kwa kuwapunguzia adha ya kutembea watoto walioko katika kata za pembezoni mwa mji na kuahidi kuendelea kuhamasisha kaya kwa kaya nakila kata wazazi waweze kupeleka watoto wao shuleni kama maagizo ya naibu waziri wa tamisemi yalivyosema kutokanana kuonekana kwa changamoto ya watoto wengi kutokufika shuleni.

Mkuu wa wilaya ya kasulu Kanal Isaac Mwakisu amesema amepokea maagizo kutoka kwa naibu waziri wa tamisemi na kuahidi kuyafanyia kazi kwa uharaka zaidi na kutoa rai kwa wananchi wote kuhakikisha wanawapeleka watoto wote kujiunga nakidato cha kwanza katika shule walizopangiwa na endapo watakaidi agizo hilo la serikali hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi ya mzazi asiye tekeleza maagizo ya serikali.

Announcements

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI JIPYA December 09, 2020
  • FOMU YA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2021 December 15, 2020
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI November 03, 2021
  • MATOKEO YA USAILI KWA NAFASI ZA UTENDAJI WA MITAA APRILI 2018 April 06, 2018
  • View All

Latest News

  • Mkuu wa Wilaya ya Kasulu atoa mikopo

    February 02, 2022
  • Mkuu wa Wilaya ya Kasulu Col. Isack Mwakisu akitoa mikopo ya Vijana, Wanawake na Walemavu toka mapato ya ndani ya Halmashauri ya Mji Kasulu

    February 02, 2022
  • NAIBU WAZIRI TAMISEMI ASISITIZA URIPOTI KIDATO CHA KWANZA

    January 23, 2022
  • NAIBU WAZIRI TAMISEMI ASISITIZA URIPOTI KIDATO CHA KWANZA

    January 22, 2022
  • View All

Video

UJENZI WA VYUMBA VYA MADARASA KUPITIA FEDHA ZA UVIKO 19 KASULU TC
More Videos

Quick Links

  • News

Related Links

  • TAMISEMI
  • Ega
  • Utumishi
  • Kigoma Region

World visitors tracker

world map hits counter

Contact Us

    Kasulu Town Council

    Postal Address: P.O.BOX 475

    Telephone: 028-2810335

    Mobile: 0784997037

    Email: td@kasulutc.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service
    • Test

Copyright ©2017 Kasulu Town Council. All rights reserved.