• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Kasulu Town Council
Kasulu Town Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Kasulu Town Council

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Strategies
  • Administration
    • Organisation Structure
    • Department
      • ELIMU SEKONDARI
      • ELIMU AWALI NA MSINGI
        • MAENDELEO YA JAMII
      • MAENDELEO YA JAMII
      • MIUNDOMBINU MAENDELEO YA MJINI NA VIJIJINI
      • HUDUMA ZA AFYA USTAWI WA JAMII NA LISHE
      • VIWANDA BIASHARA NA UWEKEZAJI
      • KILIMO MIFUGO NA UVUVI
      • MIPANGO NA URATIBU
      • UTAWALA NA USIMAMIZI WA RASILIMALI WATU
    • Units
      • USIMAMIZI WA TAKA NGUMU NA USAFI WA MAZINGIRA
      • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
      • FEDHA NA UHASIBU
      • HUDUMA ZA SHERIA
      • UKAGUZI WA NDANI
      • USIMAMIZI WA UNUNUZI
      • TEHAMA
      • MAWASILIANO SERIKALINI
      • NMALIASILI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
      • MALIASILI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
  • Investment opportunities
    • Agriculture
    • Livestock
  • Our Services
    • Health
    • Education
    • Agriculture
  • Councillors
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Ratiba
      • Ratiba
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipango Miji Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Uchumi Elimu Afya na Maji
  • Projects
    • Proposed Projects
    • On-going-Projects
    • Completed Projects
  • Publications
    • Brochures
    • By Law
    • Strategic Plan
    • Reports
  • Media Centre
    • Video
    • Press Release
    • Speeches
    • Photo Gallery

VIONGOZI WA DINI WAASWA KUTUMIA MAJUKWAA NA USHAWISHI WAO KUTOKOMEZA UKATILI KATIKA JAMII

Posted on: January 21st, 2026


Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Kasulu, Bw. Nurfus Aziz Ndee, amewataka viongozi wa dini na watu maarufu kutumia nafasi zao na ushawishi walionao kutoa elimu na kukemea vitendo vya ukatili ili kujenga jamii iliyo salama.

Wito huo umetolewa leo wakati wa ufunguzi wa kikao cha kuwawezesha viongozi wa dini na watu maarufu, kilichoandaliwa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Kasulu kupitia Idara ya Maendeleo ya Jamii – Kitengo cha Jinsia, kwa ufadhili wa UNICEF. Kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Mji wa Kasulu.

Akizungumza katika kikao hicho, Bw. Ndee aliwaasa washiriki kushiriki kikamilifu na kuwa wazi katika kufichua matendo ya ukatili yanayotokea katika jamii ili sheria ichukue mkondo wake. Aidha, aliwaomba viongozi wa dini kutoa elimu juu ya vitendo vya ukatili na kukemea vitendo hivyo, sambamba na kufundisha waumini wao kwa kuzingatia miongozo iliyotolewa na Serikali, ili kufanikisha lengo la kuwa na jamii iliyo salama.

Kikao hicho kinalenga kuwawezesha viongozi wa dini na watu maarufu kufikisha elimu ya kutokomeza vitendo vya ukatili katika jamii, hasa katika ngazi ya familia na jamii kwa ujumla. Aidha, ilielezwa kuwa si wananchi wote wanaofika katika maeneo ya ibada, hivyo kuwashirikisha watu maarufu ni njia muhimu ya kuwafikia wasiosali kupitia ushawishi wao katika jamii. Vilevile ilibainishwa kuwa si wote wanaofanya ukatili wana uelewa wa kutosha kuhusu madhara ya vitendo hivyo.

Akitoa maelezo, Afisa Maendeleo ya Jamii, Olivia Kasindu Thadeo, amesema Serikali kwa kushirikiana na wadau inalenga kujenga jamii isiyo na ukatili ili kuongeza uzalishaji na kuleta maendeleo. Alisisitiza kuwa familia zikipona, jamii nzima itapona. Aliongeza kuwa pamoja na kikao hicho, juhudi nyingine zinaendelea ikiwemo mikutano ya hadhara, utoaji wa elimu mashuleni na katika jamii.

Katika kikao hicho, washiriki walielimishwa kuhusu aina mbalimbali za ukatili ikiwemo ukatili wa kipigo, kingono, kiuchumi, kutelekezwa na kisaikolojia, huku Mkoa wa Kigoma ukitajwa kuwa miongoni mwa mikoa inayokabiliwa na changamoto ya vitendo hivyo.

Kwa upande wake, Kaimu Mchungaji wa FPCT Murusi Kasulu, Thomas Masama, aliushukuru uongozi wa Halmashauri kwa kuandaa kikao hicho na kusema mapambano dhidi ya ukatili yanahitaji ushirikiano wa wazazi, viongozi na jamii nzima, na si kuachwa kwa Serikali pekee. Alitoa wito vikao kama hivyo viendelee kufanyika na kusisitiza umuhimu wa utekelezaji wake.

Naye Kuruthum Abdallah Bishehat wa Msikiti Jabarhila Kata ya Murusi alisema mafunzo hayo yamemjengea uelewa mkubwa, hususan kwa wanawake, akisisitiza umuhimu wa wazazi kukaa na watoto wao na kuwapa elimu ya kujilinda dhidi ya hatari. Alieleza kuwa mwanamke ni nguzo ya familia, na akisimama vizuri katika nafasi yake, jamii nayo itasimama. Pia alipendekeza tathmini ifanyike kila baada ya miezi mitatu ili kupima matokeo ya elimu inayotolewa na viongozi wa dini kuhusu matendo ya ukatili.

Announcements

  • NAFASI ZA KAZI March 19, 2025
  • TANGAZO LA UBORESHAJI DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA April 30, 2025
  • TANGAZO LA KAZI July 01, 2025
  • View All

Latest News

  • VIONGOZI WA DINI WAASWA KUTUMIA MAJUKWAA NA USHAWISHI WAO KUTOKOMEZA UKATILI KATIKA JAMII

    January 21, 2026
  • MH. PROF. JOYCE NDALICHAKO AKABIDHI GARI LA WAGONJWA KITUO CHA AFYA MWAMINTARE

    December 03, 2025
  • Mkurugenzi Simbeye Apongezwa kwa Uongozi Bora kwenye Maadhimisho ya MEOS Day Kasulu TC

    November 30, 2025
  • Madiwani wapya Kuapishwa Leo

    December 02, 2025
  • View All

Video

UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA
More Videos

Quick Links

  • News

Related Links

  • TAMISEMI
  • Ega
  • Utumishi
  • Kigoma Region

World visitors tracker

world map hits counter

Contact Us

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service
    • Test

Copyright ©2017 Kasulu Town Council. All rights reserved.