• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Kasulu Town Council
Kasulu Town Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Kasulu Town Council

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Strategies
  • Administration
    • Organisation Structure
    • Department
      • ELIMU SEKONDARI
      • ELIMU AWALI NA MSINGI
        • MAENDELEO YA JAMII
      • MAENDELEO YA JAMII
      • MIUNDOMBINU MAENDELEO YA MJINI NA VIJIJINI
      • HUDUMA ZA AFYA USTAWI WA JAMII NA LISHE
      • VIWANDA BIASHARA NA UWEKEZAJI
      • KILIMO MIFUGO NA UVUVI
      • MIPANGO NA URATIBU
      • UTAWALA NA USIMAMIZI WA RASILIMALI WATU
    • Units
      • USIMAMIZI WA TAKA NGUMU NA USAFI WA MAZINGIRA
      • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
      • FEDHA NA UHASIBU
      • HUDUMA ZA SHERIA
      • UKAGUZI WA NDANI
      • USIMAMIZI WA UNUNUZI
      • TEHAMA
      • MAWASILIANO SERIKALINI
      • NMALIASILI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
      • MALIASILI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
  • Investment opportunities
    • Agriculture
    • Livestock
  • Our Services
    • Health
    • Education
    • Agriculture
  • Councillors
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Ratiba
      • Ratiba
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipango Miji Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Uchumi Elimu Afya na Maji
  • Projects
    • Proposed Projects
    • On-going-Projects
    • Completed Projects
  • Publications
    • Brochures
    • By Law
    • Strategic Plan
    • Reports
  • Media Centre
    • Video
    • Press Release
    • Speeches
    • Photo Gallery

WIZARA YA KAZI AJIRA NA WENYE ULEMAVU YAELEKEZA MIPANGO YA BAJETI 2022/2023

Posted on: August 3rd, 2022

WAZIRI WANCHI OFISI YAWAZIRI MKUU KAZI AJIRA NA WATU WENYE ULEMAVU ASOMA BAJETI YA WIZARA HIYO YA MWAKA 2022/2023 YENYE LENGO LA  KULETA USTAWI WA KIUCHUMI

Waziri wa nchi ofisi ya Waziri Mkuu kazi,ajira na watu wenye ulemavu Profesa Joyce Ndalichako amesema kuwa serikali imeanza kutekeleza mpango wa utekelezaji wa kazi mbalimbali na miradi ya maendeleo ikiwemo kusimamia masuala ya kazi na wafanyakazi nchini.

Ameyasema hayo leo julai 3 wakati akizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa Halmashauri ya Mji wa Kasulu nakuelezea mipango ya bajeti na matumizi ya wizara hiyo kwa mwaka 2022/2023 kuwa serikali ya awamu ya sita ya Raisi Samia Suluhu Hassan imedhamiria kwa dhati kuleta ustawi wa kiuchumi na kusaidia watu wenye ulemavu kwa kujenga vyuo vipya vitatu vya ufundi stadi na kuvifanyia marekebisho vituo vinne ili wawe na uwezo wa kujitegemea kiuchumi.

Aidha Ndalichako amesema kujengwa kwa vyuo hivyo kupitia bajeti ya wizara yake pamoja na ukarabati unaofanywa kutasaidia kulifanya kundi kubwa la watu wenye ulemavu kuwa na taaluma ambayo ndiyo msingi katika kuajiriwa,kujiari au kuajiri watu wengine kwenye shughuli watakazoanzisha na pia bajeti hiyo inalenga kukuza ujuzi  na utoaji wa ajira nchini ili kukabiliana na changamoto ya ukosefu wa ajira kwa vijana.

Katika kuwajenga kuweza kufanya shughuli za kiuchumi vijana 22,200 wamepatiwa mafunzo ya ujuzi wa uana genzi, vijana 3600 watapatiwa mafunzo ya ujenzi na kilimo ya kitalu nyumba kwa mikoa mitano nchini, ambapo pia vijana 500 wamepatiwa mafunzo juu ya ujuzi wa uchumi wa bluu kupitia ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba na kujenga vituo vitano kwa vijana wanaopata mafunzo ya uanagenzi.

Hata hivyo Waziri ndalichako ameendelea kusema kuwa kuendana na hali hiyo serikali kupitia wizara yake itaifanyia mapitio sera ya Taifa ya huduma na maendeleo ya watu wenye ulemavu ya mwaka 2004 ili kuweka mazingira mazuri kwa watu wenye ulemavu kushiriki shughuli za uchumi na mipango ya taifa.pamoja na utekelezaji wa mipango hiyo serikali imeanza kutekeleza mpango kabambe wa uwezeshaji kiuchumi kwa vijana kwa kuwapatia mafunzo na mitaji ili waweze kujiajiri na kutoa ajira kwa vijana wenzao.

Ndalichako amemalizia kwa kusema “mwelekeo wa bajeti kwa mwaka wa fedha 2022/2023 unalenga ukusanyaji wa maduhuli,matumizi ya kawaida na miradi ya maendeleo ambapo katika mwaka wa fedha 2022/2023 Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi,Vijana na  Watu wenye ulemavu imepangiwa kukusanya Jumla ya shilingi bilioni 45 sawa na ongezeko la asilimia 33.3kutoka shilingi bilioni  30  mwaka wa fedha wa 2021/22.’’

Announcements

  • NAFASI ZA KAZI March 19, 2025
  • TANGAZO LA UBORESHAJI DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA April 30, 2025
  • View All

Latest News

  • KAIMU KATIBU TAWALA MKOA NDUGU ELIASANTE M.MBOELO AKABIDHIWA VIFAA TIBA HUDUMA ZA MACHO MKOANI KIGOMA

    May 08, 2025
  • KAIMU KATIBU TAWALA MKOA NDUGU ELIASANTE M.MBOELO AKABIDHIWA VIFAA TIBA HUDUMA ZA MACHO MKOANI KIGOMA

    May 08, 2025
  • KAIMU KATIBU TAWALA MKOA NDUGU ELIASANTE M.MBOELO AKABIDHIWA VIFAA TIBA HUDUMA ZA MACHO MKOANI KIGOMA

    May 08, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI KASULU TC LATOA PONGEZI

    May 05, 2025
  • View All

Video

UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA
More Videos

Quick Links

  • News

Related Links

  • TAMISEMI
  • Ega
  • Utumishi
  • Kigoma Region

World visitors tracker

world map hits counter

Contact Us

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service
    • Test

Copyright ©2017 Kasulu Town Council. All rights reserved.