• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Kasulu Town Council
Kasulu Town Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Kasulu Town Council

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Strategies
  • Administration
    • Organisation Structure
    • Department
      • ELIMU SEKONDARI
      • ELIMU AWALI NA MSINGI
        • MAENDELEO YA JAMII
      • MAENDELEO YA JAMII
      • MIUNDOMBINU MAENDELEO YA MJINI NA VIJIJINI
      • HUDUMA ZA AFYA USTAWI WA JAMII NA LISHE
      • VIWANDA BIASHARA NA UWEKEZAJI
      • KILIMO MIFUGO NA UVUVI
      • MIPANGO NA URATIBU
      • UTAWALA NA USIMAMIZI WA RASILIMALI WATU
    • Units
      • USIMAMIZI WA TAKA NGUMU NA USAFI WA MAZINGIRA
      • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
      • FEDHA NA UHASIBU
      • HUDUMA ZA SHERIA
      • UKAGUZI WA NDANI
      • USIMAMIZI WA UNUNUZI
      • TEHAMA
      • MAWASILIANO SERIKALINI
      • NMALIASILI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
      • MALIASILI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
  • Investment opportunities
    • Agriculture
    • Livestock
  • Our Services
    • Health
    • Education
    • Agriculture
  • Councillors
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Ratiba
      • Ratiba
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipango Miji Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Uchumi Elimu Afya na Maji
  • Projects
    • Proposed Projects
    • On-going-Projects
    • Completed Projects
  • Publications
    • Brochures
    • By Law
    • Strategic Plan
    • Reports
  • Media Centre
    • Video
    • Press Release
    • Speeches
    • Photo Gallery

Kamati ya Uchumi,Elimu Afya na Maji


IDARA YA ELIMU MSINGI

Halmashauri ya Mji wa Kasulu ina jumla ya shule za Msingi 59 za serikali zenye jumla ya wanafunzi 55,322 kati yao wavulana 27448 na wasichana 27,874. Katika kipindi cha robo ya kwanza, 2017/2018 Idara ya Elimu Msingi imefanya kazi zifuatazo:-

· Kufanya vikao vya Kamati za shule za Mwilamvya na Mwibuye kwa ajili ya ujenzi wa vyumba 6 vya madarasa na vyoo matundu 12.

· Kufuatilia ujenzi wa madarasa 6 na matundu ya vyoo 12 katika shule za Msingi Mwilamvya na Mwibuye. Kila shule ilipata mradi wa ujenzi wa madarasa 3 na matundu 6 ya vyoo. Hali ya maendeleo ya ujenzi hadi sasa .

· Kutoa mafunzo kwa walimu 118 walimu wakuu 59 na waaratibu elimu kata 15 ya Umahiri wa kuhesabu darasa la I na II moduli ya 5-9

· Kufanya marekebisho ya taarifa za TSM na TSA kila kwenye mfumo BEMIS.

· Kuendelea kutoa huduma za kitaaluma na kitaalamu kwa wateja mbalimbali wanaofika ofisini.

· Kuendelea kusimamia utekelezaji wa sera ya ‘’ELIMU BURE’’ kwa wanafunzi wote wa Elimu ya msingi.

· Kusimamia na kufuatailia usafi katika kituo cha Elimu maalum Kabanga.

· Kufanya maandalizi ya mwisho ya Mtihani wa Taifa wa Kumaliza Elimu ya Msingi (PSLE) 2017 pamoja na kufanyika kwa mtihani huo. Maandalizi yaliyofanyika ni pamoja na:-

- Kuandaa vikao vya kamati ya Uendeshaji Mitihani ngazi ya wilaya na Mkoa.

- Kugawa baadhi ya vifaa muhimu kama vile vibao, rubber band na CAL.

- Kufanya uteuzi wa wasimamizi wa Mtihani na kuwasilisha mkoani.

- Kuchukua mtihani wa Taifa wa Kumaliza Elimu ya Msingi kutoka Mkoani kuja Halmashauri..

- Kuandaa bajeti ya Mtihani.

- Kuandaa malipo kwa wasimamizi.

- Kufanya semina ya maelekezi kwa wasimamizi.

- Kutawanya mitihani na wasimamizi katika vituo vya mitihani n.k.

· Kufanyika kwa Mtihani wa Taifa wa Kumakiza Elimu ya Msingi tarehe 06 – 07/09/2017.Taarifa ya watahiniwa ilikuwa kama ifuatavyo:-

WALIOSAJILIWA

WALIOFANYA MTIHANI

%

WASIOFANYA MTIHANI

%

WAV

WAS

JML

WAV

WAS

JML

WAV

WAS

JML

1950
2293
4243
1942
2280
4222
99.5
8
13
21
0.5

· Kuhakiki watumishi hewa. Ni zoezi linalofanyika kila mwezi kwa kutumia Pay roll.

  • Kuandaa taarifa ya LAAC ya Idara ya Elimu Msingi.

· Kukusanya madai mbalimbali ya watumishi walimu yasiyo mishahara.

· Kuendesha mafunzo kwa Walimu wakuu, walimu wa miradi shuleni wajumbe mmoja moja wa kamati za shule na Mfanyabiashara mmoja mmoja kutoka kila Mtaa. Mafunzo hayo yaliendeshwa na kuwezeshwa na Eguip-Tanzania.

· Kuhudhuria semina ya ugawaji wa vyandarua kwa wanafunzi wa darasa la I -III Mkoa wa Kigoma.

· Kuhamisha na kupokea wanafunzi wanaohama ndani na nje ya Halmashauri.

· Kukusanya takwimu za Walimu kwa majina yao toka kila shule. Zoezi hili lilifanyika hadi Agosti, 2017.

· Kutembelea shule ili kuona hali ya ufundishaji inavyoendelea Shule za Juhudi, Mwenge, Mwilamvya, Nyarumanga, Kanazi na Nyakabondo zimetembelewa.

· Kutembelea shule za Kiganamo, Bogwe, Kalema, Uhuru, Murubona na Umoja ili kuona hali ya utekelezaji wa Mtaala mpya ulioboreshwa.

· Kuhudhuria semina ya Early Grade Mathematics (EGM) iliyoyanyika Kigoma kuanzia Tarehe 1 – 5 /8/2017.

· Kufanya ukaguzi na ufuatiliaji wa huduma za maji, Elimu Afya na usafi wa Mazingira shuleni kwa shule 88 za Msingi na sekondari.

IDARA YA ELIMU SEKONDARI

Idara ya Elimu Sekondari inasimamia shughuli za maendeleo katika Shule 25 za Sekondari, kati ya shule hizo, 11 ni za Serikali na 14 ni shule zisizo za serikali. Idara ina jumla ya walimu 299, Fundi sanifu Maabara 1 na maafisa 4. Idara imetekeleza majukumu yake kwa kipindi cha mwezi April – June, 2017 kwa kuzingatia Mpango Kazi wa Idara 2017/2018 kama ifuatavyo;

 

2. SHUGHULI NILIZOTEKELEZA 

2.1 KUSHIRIKI UENDESHAJI NA USIMAMIZI WA MTIHANI YA KUHITIMU ELIMU YA MSINGI

Idara ya elimu sekondari ilishiriki kikamilifu katika usimamizi na uendeshaji wa Mtihani wa Kumaliza Elimu ya Msingi PSLE 2017.

2.2 UHAKIKI MADENI YA WALIMU

Idara kwa kushirikiana na timu ya uhakiki wa madeni ya wilaya ilihakiki madeni ya walimu yasiyokuwa ya mishahara kuanzia julai 2016 hadi Juni 2017 na kuyawasilisha mamlaka za juu Mkoa na Wizara.

2.3 KUKUSANYA NA KUJAZA TAKWIMU MBALIMBALI ZA ELIMU KUTOKA SHULENI NA KUZIWASILISHA KATIKA MAMLAKA HUSIKA

Idara ilikusanya takwimu mabalimbali katika shule za sekondari na kuandaa taarifa mbalimbali kulingana na maelekezo na kuziwasilisha katika mamlaka husika

  • Idadi ya wanafunzi, mikondo na walimu wanaofundisha kwa masomo.
  • Taarifa za miradi ya ujenzi ya P4R.
  • Kusahihisha taarifa za BEMIS.
  • Taarifa za LAAC.
  • Takwimu za watahiniwa wa kidato cha nne, maarifa na kidato cha pili.
  • Uchambuzi wa matokeo ya Mithani ya Taifa.

2.4  KUFANYA MAANDALIZI YA MTIHANI WA KIDATO CHA PILI NA CHA NNE MWAKA 2017

Idara imefanya maandalizi ya ufanyikaji wa mitihani ya kidato cha Pili (FTNA), Nne na Maarifa (CSEE & QT), 2017. Mitihani hii inatarajiwa kuanza kufanyika mwishoni mwa mwezi Oktoba na Novemba 2017.

2.5 KUSIMAMIA UENDESHAJI WA MTIHANI YA UTIMILIFU WA KIDATO CHA NNE (MOCK ) MKOA, NA PRE NATIONAL, 2017 

Idara iliratibu maandalizi na ufanyikaji wa mitihani tajwa hapo juu yaani uandaaji wa bajeti, uteuzi wa walimu wa kutunga, kuhakiki, usimamizi wa ufanyikaji, usahihishaji na utoaji wa matokeo ya mtihani na matokeo yalikuwa kama kiambatisho kinavyoonesha. Mtihani wa Pre-National ulifanyika ili kuongeza mazoezi kwa watahiniwa wa shule za serikali na kuwa tayari katika ushindani kwa kufanya mitihani ambayo haikutungwa na walimu wanaofundisha masomo yao.

2.6 KUSIMAMIA UUNDWAJI WA ZA BODI ZA SHULE

Idara ilitoa maelekezo ya namna ya kupendekeza wajumbe wa Bodi za shule kwa shule zote za serikali na zisizo za serikali ambazo Bodi zao ziliisha muda wake ama zilikuwa hazina Bodi na kuhakikisha mapendekezo yote yamepelekwa katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Kigoma.

2.7 KUFANYA UFUATILIJI WA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI 

KATIKA SHULE ZA SEKONDARI

Kufanya ufuatiliaji wa ufundishaji na ujifunzaji katika shule za sekondari na kutoa ushauri.

2.8 UWEKAJI WA JIWE LA MSINGI KATIKA SHULE YA KIGOMA GRAND

Idara ilishiriki taratibu zote za maandalizi katika uwekaji wa jiwe la msingi katika shule ya KIGOMA GRAND tarehe 19 august, 2017. Jiwe la msingi liliwekwa na Mhe.Prof. Joyce Ndalichako (MB), Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia.

2.9 KUENDESHA VIKAO MBALIMBALI VYA KIUTENDAJI

Idara iliendesha vikao kwa ajili ya uboreshaji wa utekelezaji wa majukumu ya kutoa elimu ya sekondari kwa wakuu wa shule za serikali na zisizo za serikali. Vikao hivyo ni kikao cha mrejesho wa

2.10 Kuhudhuria vikao vya Bodi za shule na kutoa ushauri wa changamoto mbalimbali

3.0 MAPOKEZI YA FEDHA

Idara ya Elimu Sekondari katika kipindi cha Robo ya Kwanza ya Julai– Septemba 2017/2018 Imepokea fedha Tsh. 73,201,775.09 na kutekeleza shughuli mbalimbali kwa mchanganuo ufuatao katika jedwali;

Na.
MUDA WA KAZI
SHUGHULI ILIYOFANYIKA
PESA ILIYOPOKELEWA
1.
Julai
Mgawo wa Elimu Bure
36,600,357.09
2
Augost
Mgawo wa Fedha za elimu bila malipo
36,601,424
3
Septemba

73,201,775.09

IDARA YA MAENDELEO YA JAMII

Taarifa ya idara ya maendeleo ya jamii ya robo ya kwanza. Katika taarifa hii imegawanyika katika sehemu zifuatazo; Taarifa ya uhakiki wa asasi zisizo za kiserikali (NGOs) ,Taarifa ya mfuko wa wanawake (WDF), na Taarifa ya vikundi vilivyosajiliwa.

Kwa mwaka wa fedha 2017/2018 katika robo ya kwanza, Halmashauri ya Mji wa Kasulu imefanikiwa kisajili vikundi 25 vya wanawake na vijana. Vikundi hivi vinajishughulisha na shughuli mbalimbali za uzalishaji mali kama vilivyoorodheshwa hapa chini:

Na
JINA LA KIKUNDI
NAMBA YA USAJILI
MAHALI KILIPO
TAREHE YA USAJILI
SHUGHULI ZA KIKUNDI
1
Chama cha madereva mchomoko
KTC /CBO/0099
MURUBONA
16.07.2015
Kusafirisha abiria ndani na nje ya mji wa kasulu
2
AMANI WOMEN
KTC /CBO/0103
KUMSENGA
22.07.2017
Kununua na kuuza mazao
3
NIYOKURU WAJANE WOMEN GROUP
KTC /CBO/0104
NYANSHA
30.7.2017
Kununua na kuuza mazao ya chakula
pamoja na kilimo cha bustani.
4
KILOMBERO YOUTH GROUP
KTC /CBO/0106
MURUSI
12.8.2017
Kupakia mizigo ya mazao ya tumbaku
5
ILAKOZE GROUP WANAWAKE
KTC /CBO/0105
MURUSI
12.8.2017
Mazao ya chakula
6
TUPENDANE KWA SHAYO WANAWAKE
KTC /CBO/0107
MURUSI
16.8.2017
Kuweka na kukopa, kusaidiana katika shida na raha
7
NNUUR-ISLAMIC WOMEN GROUP
KTC /CBO/0109
MWILAVYA
16.8.2017
Kuweka na kukopa
8
KASULU TUMAINI HISA GROUP
KTC /CBO/0111
KUMSENGA
17.8.2017
Kuweka na kukopa
9
KASULU NEEMA GROUP
KTC /CBO/0110
KUMSENGA
17.8.2017
Kuweka na kukopa
10
TWENDE NA WAKATI WANAWAKE
KTC /CBO/0108
MURUFITI
21.8. 2017
Kutoa elimu ya ujasiliamali
11
JITEGEMEE VIKOBA
KTC /CBO/0112
HERU-JUU
19.8.2017
Kuweka na kukopa
12
UPATANISHO VIJANA GROUP
KTC /CBO/0113
MURUSI
21.8.2017
Uuzaji na ununuzi wa mazao
13
FURAHA WOMEN
KTC /CBO/0114
MURUSI
21.9.2017
Uuzaji wa duka la dawa muhimu
14
TUINUANE WALEMAVU GROUP
KTC /CBO/0115
NYANSHA
11.9.2017
Ufugaji wa nguruwe
15
KILIMO KWANZA WANAWAKE
KTC /CBO/0116
MURUSI
11.9.2017
Kilimo cha mihogo
16
EFSA WOMEN GROUP
KTC /CBO/0117
MURUSI
11.9.2017
Uuzaji wa chakula hotel
17
TUMAINI NYAKALELA
KTC /CBO/0118
HERU-JUU
11.9.2017
Ufugaji wa kuku wa kienyeji ujasiliamali kilimo cha mazao ya chakula
18
EDENI WOMEN GROUP
KTC /CBO/0120
MURUSI
11.9.2017
Ununuzi na uuzaji wa mazao
19
COMPLEX ACT YOUTH GROUP
KTC/CBO/0121
MURUSI
11.09.2017
Sanaa ya uingizaji ,ufugaji wa kuku wa mayai
20
SAYUNI WOMEN GROUP
KTC/CBO/0122
MURUSI
11.09.2017
Kuuza na kununua mazao ya chakula
21
ZANTEL YOUTH GROUP
KTC/CBO/0123
NYUMBIGWA
12.09.2017
Kilimo cha matunda
22
MAANDARIO WOMEN
KTC/CBO/0124
MURUSI
26.29. 2017
Kuuza na kununua mazao ya chakula.
23
VIJANA WAFUGA BATA
KTC/CBO/0125
MWILAVYA
28.09.2017
Ufugaji bata.
24
JITIHADA WOMEN GROUP
KTC/CBO/0126
KUMSENGA
14.03.2017
Kuweka na kukopa na kilimo cha chakulaovyamaji.
25
SHALOOM WOMEN GROUP
KTC/CBO/0127
MURUSI
29.09.2017
Uuzaji wa mbegu na mboleafirishaabirianamizigoyao.

 MASHIRIKA YA SIYO KUWA YA KISERIKALI (NGOs) YALIYO HAKIKIWA NAKUTAMBULIWA KUFANYAKAZI KATIKA HALMASHAURI YA MJI WA KASULU .

Katika Halmashauri ya mji wa Kasulu kuna mashirika 15 yasiyo ya kiserikali (NGOs) yanayotambuliwa na Idara ya Maendeleo ya Jamii. Mashirika haya yanatoa huduma zake ndani na nje ya mipaka ya Halmashauri ya mji wa Kasulu. Baadhi ya mashirika haya yanatoa huduma zake kwa wakimbizi. Aidha mashirika yanayotolewa taarifa zake ni yale ambayo walileta utambulisho na yamekuwa yakileta taarifa zao za utekelezaji. Mashirika hayo yameorodheshwa hapa chini.

TAARIFA YA NGOs ZINAZOFANYAKAZI KATIKA HALMASHAURI YA MJI.

N/S
JINA LA NGOs
MAHALI ILIPO/ENEO LA OFISI
KAZI /SHUGHILI ZA NGOs
NAMBA ZA NGOs
MWAKA WA WAKUANZA
1
WESTERN TANGANYIKA ENTERPRENEUR IN AGRICULTUREBAND FISH CAPTIVITY ORGANIZATION (WETAAIFICO)
MKOA WA KIGOMA , WILAYA YA KASULU, MTAA WA MRUSI
KUJENGA UJUZI WA VITENDO KATIKA KILIMO , UFUGAJI WA WANYAMA NA SAMAKI. UFUGAJI WA NYUKI NA USINDIKAJI WA CHAKULA (NK)
OONGOs/00004592
15/07/2010
2
CONSORTIUM
KASULU TC MURUSI
KUTUNZA MAZINGIRA ,KUWAPATIA ELIMU YA KIAFYA KWA JAMII
No S. A 17243
24TH JANUARY, 2011
3
SAVE FOR DEVELOPMENT AND RELIEF ASSOCIATION(SADERA)
KASULU TC KIGANAMO
KUTOA ELIMU YA AFYA KWA JAMII YA KASULU MJINI NA VIJIJINI. KU WEZESHA VIKUNDI VYA WA NAWAKE NA VIJANA WA KIKE NA KIUME KIUCHUMI.
00NGOs/ 00001461
12/03/2012
4
TREECOVER FOUNDATION (TCF)
KASULU TC BARABARA YA KIBONDO MKABARA NA OFISI YA HALMASHAUR YA MJI.
UTUNZAJI WA MAZINGIRA PAMOJA NA KUANDAA VITARU VYA MITI.
OONGOs/ 0009245
29TH MAY 2017
5
WAKWANZA PARALEGAL ORGANIZATION (WAPAO)
KASULU TC MURUSI
KUELIMISHA JAMII JUU YA MASUALA KISHERIA NA HAKI ZA KIJAMII PAMOJA NA KUSURUHISHA MIGOGORO YA KIJAMII.
06/NGOs/08451.

6
HAKI ORGANIZATION
KASULU TC MTAA WAMISSION AGRICANA
KUTOA HUDUMA ZA KISHERIA KWA WTOTO WA MITAANI , MITAA, WAJANE NA MAYATIMA.
SO. NO. 11963
11TH AUGUST 2003
7
TANZANIA AGRICULTURE AND ENVIROMENT DEVELOPMENT ORGANIZATION, (T,A.E.D.O)
KASULU T.C MRUVUMU
KUTUNZA MAZINGIRA,KUOTESHAJI WA MITI NA UPANDAJI MITI PAMOJA NA KILIMO CHA MSETO KWA KUTUMIA MITI INAYORUTUBISHA ARTHI NA MBOLEA YA SAMADI NA MBOJI
SO.14983.
2 AUGUST2004
8
TANZANIA RURAL DEVELOPMENT AND RELIEF ORGANIZATION (TARUDEREO)
KASULU TC
T.T.C
KUTOA HUDUMA KUSAIDIA WANAWAKE NA VIJANA PAMOJA NA WAKIMBIZI WALIO ATHIRIKA KIJAMII HASA WALE WA LIO MAKAMBINI
SO NO 11470

9
FIGHTERS FOR DEVELOPMENT SUSTAINABILITY (FIDESU)

UTUNZAJI WA MAZINGIRA ,UOTESHAJI WA MICHE YA MITI, AFYA , KILIMO, UFUGAJI WA NYUKI , UFUGAJI WA SAMAKI,KUKU, NA KILIMO CHA MIWA NA MIHOGO.
OONGOs/08593
16TH MAY 2016
10
KASULU MOBILE EYE CARE FOUNDATION(KAMECAF)
KASULU T.C
KWIZERA
KUELIMISHA JAMII KUHUSU MAGONJWA YA MACHO NA KUTOA MATIBABU YAKE.
00NGO/0008800
25TH OCTOBER/2016
11
DISABILITY RELIEF SERVICES (DRS)- TANZANIA
KASULU TC MATAA WA KWIZERA
KUTOA HUDUMU ZA VIWEZESHA (SUPPORTING GEAR) KWA WATU WENYE ULEMAVU KASULU MJINI NA VIJIJINI ILI KUWALAHISHIA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU YAO YA KIMAISHA. KUWAJENGEA

January 2016
12
BENEVOLENT INSTITUTE OF DEVELOPMENT INITIATIVE IN TANZANIA,(BIDII-TANZANIA)
KASULU T.C MTAA WA NYASHA
KUTOA MAFUNZO KWA WAKULIMA NA JUU YA MIFUNGO,KUHUSU UFUNGAJI BORA WA NGOMBE WA MAZIWA NA NYAMA YA NGURUWE,MBUZI NA KUKU , NA PAMOJA NA KILIMO BORA CHA MAZAO YA CHAKULA ,
SO. 12676
AUGUST 2004
13
KASULU HEALTH HOME BASED CARE ORGANIZATION (KAHHOBACO)
KASULU T.C
MTAA WA NYASHA
CLINIC YA AFYAYA UZAZI NA MTOTO PAMOJA NA KUTOA ELIMU YA JAMII JUU YA KUZUIA MAGONJWA MBALI MBALI KAMA VILE MALARIA NA HIV/AIDS
OO NGO/ 00003052
08TH APRIL 2009
14
TANZANIA HELP ELDERLY AND SINGLE PARENT ORGANIZATION (THESPO)
KASULU T.C
JIRANI NA KANISA KUU LA ANGLICANA
KUSAIDIA WATOTO WANAOISHI KATIKA MAZINGIRA HATARISHI PAMOJA NA KUSAIDIA YATIMA , WAJANE NA WAZEE. KUTOA ELIMU KWA JAMII KUHUSIANA NA MAGONJWA MBALI MBALI IKIWEMO MAGONJWA YA MLIPUKO PAMOJA NA MAZINGIRA.
00NGO/00007863
5TH MARCH 2015
15
SAIDIA WAZEE (SAWATA)
KASULU T.C
UJENZI
KUTOA HUDUMA ZA KUSAIDIA WAZEE KWA AJILI YA KUINUA MAISHA YAO NA KUPUNG O MISONGO YA WAZEENI
SO.NO .8039
16/10/2008
16
AMENITY NON PROFIT CHARITY ORGANIZATION (ANCO)
KASULU T.C
MURUBONA MTAA WA UMOJA
UWEZESHAJI WANAWAKE KIJAMII NA KIUCHUMI PAMOJA NA ILINZI WA HAKI NA USTAWI WA WATOTO
O6NGO/00005896
19TH OCTOBER 2012

 

 MAPENDEKEZO YA VIKUNDI VINAVYOTEGEMEWA KUPATA MIKOPO 

s/n
Jina la kikundi
Kata 
kiasi
Mradi wa kikundi
1.
Bwiza women
Murusi
2,000,000
Ufugaji wa kuku
2.
Tupendane women Kwa Shayo group
Murusi
2,000,000
Uuzaji wa mazao
3.
Tuinuane walemavu group
Nyansha
2,500,000
Ufugaji wa nguruwe
4.
Tuhudumiane wajane
Nyansha
3,000,000
Kilimo cha bustani ,kuweka na kukopa
5
Itangigomba women
Kumsenga
3,000,000
Ununuzi na uuzaji wa mazao
6
Furaha women
Murusi
3,000,000
Duka la dawa baridi
7
Kayore youth
Murubona
3,000,000
Mradi wa kutengeneza viatu
8
Mshikamano women
Murubona
4,000,000
Kutengeneza sabuni za maji na masweta
9
Amani women
Kumsenga
2,000,000
Kulangua mazao na kuuza
10
Niyonkuru wajane
Murubona
2,500,000
Kununua na kuuza mazao

Jumla

27,000,000

IDARA YA KILIMO NA UMWAGILIAJI

Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika Mji ina jumla ya watumishi 12,kati ya hao watumishi 2 wako ngazi ya ofisi kuu na 10 ngazi ya kata na mtaa.Katika kipindi cha robo ya kwanza cha mwaka wa fedha 2017/18 katika kipindi hiki idara ilitekeleza shughuli kusimamia na kufuatilia ujenzi wa soko la sofya .paomoja na shughuli za ugani kama zilivyoainishwa hapa chini.

HALI YA HEWA.

 Katika Kipindi cha robo ya kwanza kimekuwa cha kiangazi ambacho wakulima walikitumia kuzalisha mazao ya bustani hasa mboga za majani ,mahindi na maharage maeneo ya bondeni yenye ardhi oevu.

PEMBEJEO ZA KILIMO

Mwaka huu wa fedha 2017/18 serikali haitatoa ruzuku za pembejeo kwa mfumo wa vocha kama ilivyofanyika kwa miaka ya nyuma badala yake serikali imeelekeza wakala wa pembejeo kutoa bei elekezi kwa mbolea ya kupandia aina ya DAP kuwa itauzwa kwa sh.56,000 badala ya sh 65,000 inayouzwa na wafanyabiashara katika Halmashauri ya Mji wa Kasulu na Urea Kuuzwa kwa sh 43,679 badala y ash.48,000 iliyopo madukani sasa.

 4.SHUGHULI ZA UGANI.

Katika msimu wa Kilimo 2017/18 idara ya kilimo imepanga kutekeleza shughuliza

Kwa kuzingatia malengo yafuatayo:-

MALENGO YA KILIMO MSIMU 2017/18 

ZAO
LENGO(HEKTA)
UVUNAJI
TANI
MAHINDI
30,000
52,500
JUMLA NDOGO
 
30,000
52,500
MAHARAGE
5950
29,750
MBAAZI
105
105
NJEGERE
12.5
12.5
JUMLA NDOGO
6067.5
2,929
MIHOGO
8960
89,600
VIAZI VITAMU
399
3,192
VIAZI MVIRINGO
70
595
MAGIMBI
18
180
JUMLA NDOGO
9,447
93,567
VITUNGUU SAUMU
10
75
TANGAWIZI
9
90
 
JUMLA NDOGO
 
19
 
165
NYANYA
90
2250
VITUNGUU
62
465
HOHO
28
28
KABICHI
38
760
MCHICHA
21
21
CHINESE KABICHI
7
7
KAROTI
5
20
NYANYA CHUNGU
14
72
MATANGO
6
24
TIKITI
8
80
JUMLA NDOGO
269
3,727
KAHAWA
20
13
ALIZETI
35
-
KARANGA
95
95
NDIZI MBIVU
37
225
NDIZI MBICHICHI
98
450
MIWA
59
590
JUMLA
361
1,360
MALIMAO
12
12
MACHUNGWA
16
32
CHENZA
6
12
AVOCARDO
5
50
PAPAI
12
120
PASHENI
5
5
JUMLA NDOGO
56
231
JUMLA KUU
46,219
154,479

IDARA YA MAJI 

TAARIFA YA UTEKELEZAJI YA IDARA YA MAJI KWA ROBO YA KWANZA

Katika Robo hii ya kwanza Idara ya Maji iliendelea kusimamia ujenzi wa miradi ya maji Kimobwa,Heru juu na Muhunga. Utekelezaji wa miradi hiyo ipo katika hatua mbalimbali ambapo mradi wa maji Heru juu umekamilika kwa 75%, Mradi wa Maji kimobwa umekamilika kwa 79% na Mradi wa maji Muhunga umekamilika kwa 70%. Wakazi katika miradi ya maeneo yote matatu wameanza kunufaika na huduma ya maji kupitia miradi hiyo.Hata hivyo miradi hiyo ilitarajia kukamilika tarehe 09/11/2017 kama fedha ingekuja kwa wakati.Mpaka kufikia hatua hiyo mkandarasi alikuwa amelipwa asilimia 15 ya fedha zote za utekelezaji wa mradi.Mkandarasi katika miradi ya Heru-Juu na Kimobwa ameomba kuongezewa muda wa mwezi mmoja kwani fedha ya miradi hiyo imengia tarehe 02.11.2017 na mkandarasi wa mradi wa muhunga ameomba kuongezewa miezi 2 kwasababu anatakiwa kujenga tenki la Maji ambalo litatakiwa kukaa na maji kwa siku 21 kabla ya kufunikwa.

Vilevile katika Robo hii Idara ya Maji iliendeleza zoezi la kuunda na kusajili vyombo vya Watumia maji. Vyombo vya watumia Maji vimeundwa katika maeneo ya Kanazi, Ruhita, Heru juu, Mwanga B, Nyumbigwa, Kabanga na Msambara. Utaratibu wa kuvisajili umekamilika kwa maeneo ya kabanga na Msambara. Usajili kwa maeneo yaliyobakia umekamilishwa katika Robo ya pili ya mwaka 2017/18.

Changamoto kubwa zinazokabili Idara ya maji hivi sasa ni uzalishaji wa maji mdogo kuliko mahitaji ya maji kwa Wakazi wa Halmashauri ya mji wa Kasulu. Wakazi wanaopata huduma ya maji ni 58%. Katika kukabiliana na Changamoto hili, Mipango ya utekelezaji wa Miradi umeandaliwa na utekelezaji wake umepangwa kufanyika kwa kipindi cha miaka mitano kati ya 2016 -2021. Ujenzi wa miradi ya maji inayoendelea katika maeneo ya kimobwa, Heru juu na Muhunga ni sehemu ya utekelezaji wa mpango hiyo.

Changamoto ingine ni Uhaba wa Watumishi katika sekta ya Maji. Idara ina watumishi 4 ambao ni waajiriwa ikilinganishwa na mahitaji halisi ya watumishi 21. Upungufu huo wa jumla ya watumishi 17 unapunguza kasi na ufanisi katika utoaji wa huduma ya Maji. Maombi kuonesha hitaji la watumishi wapya yamewasilishwa TAMISEMI na ufuatiliaji unaendelea. 

Announcements

  • NAFASI ZA KAZI March 19, 2025
  • TANGAZO LA UBORESHAJI DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA April 30, 2025
  • View All

Latest News

  • Mkurugenzi Simbeye Aamsha Ari Mpya Kasulu Mji: Aanzisha Timu za Michezo kwa Watumishi, Aweka Historia Mpya ya Ushirikiano Kazini.

    May 17, 2025
  • BOOST YABORESHA ELIMU YA AWALI KASULU

    May 16, 2025
  • KAIMU KATIBU TAWALA MKOA NDUGU ELIASANTE M.MBOELO AKABIDHIWA VIFAA TIBA HUDUMA ZA MACHO MKOANI KIGOMA

    May 08, 2025
  • KAIMU KATIBU TAWALA MKOA NDUGU ELIASANTE M.MBOELO AKABIDHIWA VIFAA TIBA HUDUMA ZA MACHO MKOANI KIGOMA

    May 08, 2025
  • View All

Video

UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA
More Videos

Quick Links

  • News

Related Links

  • TAMISEMI
  • Ega
  • Utumishi
  • Kigoma Region

World visitors tracker

world map hits counter

Contact Us

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service
    • Test

Copyright ©2017 Kasulu Town Council. All rights reserved.