• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Kasulu Town Council
Kasulu Town Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Kasulu Town Council

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Strategies
  • Administration
    • Organisation Structure
    • Department
      • ELIMU SEKONDARI
      • ELIMU AWALI NA MSINGI
        • MAENDELEO YA JAMII
      • MAENDELEO YA JAMII
      • MIUNDOMBINU MAENDELEO YA MJINI NA VIJIJINI
      • HUDUMA ZA AFYA USTAWI WA JAMII NA LISHE
      • VIWANDA BIASHARA NA UWEKEZAJI
      • KILIMO MIFUGO NA UVUVI
      • MIPANGO NA URATIBU
      • UTAWALA NA USIMAMIZI WA RASILIMALI WATU
    • Units
      • USIMAMIZI WA TAKA NGUMU NA USAFI WA MAZINGIRA
      • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
      • FEDHA NA UHASIBU
      • HUDUMA ZA SHERIA
      • UKAGUZI WA NDANI
      • USIMAMIZI WA UNUNUZI
      • TEHAMA
      • MAWASILIANO SERIKALINI
      • NMALIASILI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
      • MALIASILI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
  • Investment opportunities
    • Agriculture
    • Livestock
  • Our Services
    • Health
    • Education
    • Agriculture
  • Councillors
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Ratiba
      • Ratiba
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipango Miji Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Uchumi Elimu Afya na Maji
  • Projects
    • Proposed Projects
    • On-going-Projects
    • Completed Projects
  • Publications
    • Brochures
    • By Law
    • Strategic Plan
    • Reports
  • Media Centre
    • Video
    • Press Release
    • Speeches
    • Photo Gallery

DC MWAKISU AWATAKA WATENDAJI KUFANYA KAZI KWA UADILIFU

Posted on: March 27th, 2025

Hayo yamesemwa na Mkuu wa wilaya ya Kasulu Kanal Isaack A.Mwakisu wakati akifungua mafunzo maalumu kwa watendaji wote wa kata zote za wilaya ya Kasulu pamoja na maafisa tarafa kwaajili ya kuwajengea uwezo na kuwakumbusha uwajibikaji katika maeneo yao ya kazi.

Katika hotuba yake ya ufunguzi wa mafunzo hayo yaliyohudhuriwa pia na Katibu tawala,Mkuu wa Jeshi la Polisi,DC Mwakisu amesema sura ya serikali inaonyeshwa na watendaji katika maeneo yao ya kazi na hivyo ni vyema kuhakikisha wanatumika kwa weredi na uadilifu mkubwa katika utendaji wa shughuli zao za kila siku.

DC Mwakisu amekemea suala la baadhi ya watendaji  kutoa vitisho kwa wananchi  na kusema vitendo vya namna hii vinaondoa sifa nzuri ya serikali na kuwafanya wananchi  wasiwe na ujasiri wa kueleza matatizo yao na hii kupelekea serikali kulaumiwa kutokana na kuwepo kwa migogoro mingi isiyotatuliwa.

Amesisitiza suala la ushirikiano na viongozi wengine wa serikali kama polisi kata na wengine na kusema kiongozi ni mtu anayeongoza wengine lakini pia naye anahitaji kuongozwa hivyo hauwezi kufanya kazi peke yako bila ushirika na watu anaowaongoza na pia kutoka  kwa viongozi wengine.

Aidha DC Mwakisu amekemea suala la ‘’uboss ‘’katika maeneo yao ya kazi na kuwashauri wafuate maadili na kupendana na kuheshimiana wakimhudumia kila mtu kwa usawa na heshima pamoja na uadilifu.

DC amewatakia mafunzo mema na kuwataka wazingatie mafunzo yatakayotolewa na kwamba wanatakiwa kuhakikisha wanatekeleza yote watakayofundishwa kwa ajili ya ustawi wa jamii yetu na kuwapa imani wananchi kwa serikali yao inayofanya kazi kubwa kuwatumikia wananchi wao.

Suala la watendaji kukaa maeneo yao ya kazi ni suala ambalo pia DC Mwakisu amewaagiza na kusema ni jambo la msingi sana kiongozi kukaa eneo lake la kazi ili kuwapa uwezo wa kuyajua matatizo ya wananchi na hasa kwa mwaka huu wa uchaguzi "Nendeni mkakae katika maeneo yenu ya kazi achene kukaa mjini wakati wananchi wanahitaji kuhudumiwa,mtambue kwamba mmeaminiwa na Serikali kati ya watanzania wengi”.

Kwa upande wake Katibu tawala Wilaya ya Kasulu Bi Theresia Mtewele amewataka Watendaji na Maafisa Tarafa kujua mipaka ya uongozi na kuzingatia maadili ili kufikia malengo ya kinidhamu katika kudumisha utumishi wenye weledi, kujua mipaka ya uongozi na kuwa makini katika kufanya maamuzi hasa wakati wa utatuzi wa migogoro Kwa wananchi ili kujiepusha na migogoro baina ya mwajiri na Jamii wanayoihudumia.

Akitoa mada ya kwanza ya "Mjue Jirani yako" Afisa Uhamiaji Bi.Restuta amewashukuru watendaji wanaoendelea kutoa ushirikiano kwa Ofisi ya Uhamiaji na kuwaeleza kwamba wanategemea sana taarifa mbalimbali kama vile za wahamiaji haramu kutoka kwao na kuwaomba

Aidha bi Restuta  amewataka watendaji kuhakikisha taratibu za kisheria zinafuatwa wakati wa kufanya operation yoyote  inayohusiana na mambo ya uhamiaji ikiwa ni pamoja na kuhakikisha wanashirikiana kwa karibu na Jeshi la  Uhamiaji.

Kwa upande wake SSP Athmani Issango OCD wilaya ya Kasulu akiwasilisha mada ya pili iliyohusu Ulinzi na Usalama  amewataka watendaji kujua wajibu walionao na mamlaka yao kwa mujibu wa sheria katika kutekeleza majukumu yao hususani katika kusimamia ulinzi na usalama wa raia na mali zao ili kuepuka uvunjaji wa sheria.

Aidha ameshukuru ushirikaano unaoendelea kati ya jeshi la polisi na watendaji pamoja na maafisa tarafa katika kupambana na uhalifu na hivyo kufanya Wilaya ya Kasulu kuwa shwari na watu kuendelea kufanya kazi zao kwa amani.

Katika mafunzo hayo watendaji walipata wasaa pia kujifunza juu ya maada mbalimbali ikiwemo wajibu wa Serikali katika kupambana na kuzuia rushwa iliyowasilishwa na Alpha Eliatosha Afisa kutoka Takukuru ,Kanuni za utumishi wa umma ambayo iliwasilishwa na katibu tawala wa wilaya bi Theresia Mtewele pamoja na afisa utumishi Halmashauri ya Mji Kasulu Daniel Kaloza.

Announcements

  • NAFASI ZA KAZI March 19, 2025
  • TANGAZO LA UBORESHAJI DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA April 30, 2025
  • TANGAZO LA KAZI July 01, 2025
  • View All

Latest News

  • MPANGO WA SHULE BORA IMEBORESHA TAALUMA YA UFUNDISHAJI KASULU MJINI.

    July 01, 2025
  • JAI SHUJAA WA DAMU KASULU

    June 09, 2025
  • “Waalimu Waaswa Kuongeza Ubunifu Katika Kufundisha Ili Kuleta Mabadiliko Chanya”;TD Simbeye.

    May 30, 2025
  • Waajiriwa Wapya wa Halmashauri ya Mji Kasulu Wajengewa Uwezo Kupitia Mafunzo ya Mfumo wa MUKI

    May 29, 2025
  • View All

Video

UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA
More Videos

Quick Links

  • News

Related Links

  • TAMISEMI
  • Ega
  • Utumishi
  • Kigoma Region

World visitors tracker

world map hits counter

Contact Us

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service
    • Test

Copyright ©2017 Kasulu Town Council. All rights reserved.