• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Kasulu Town Council
Kasulu Town Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Kasulu Town Council

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Strategies
  • Administration
    • Organisation Structure
    • Department
      • ELIMU SEKONDARI
      • ELIMU AWALI NA MSINGI
        • MAENDELEO YA JAMII
      • MAENDELEO YA JAMII
      • MIUNDOMBINU MAENDELEO YA MJINI NA VIJIJINI
      • HUDUMA ZA AFYA USTAWI WA JAMII NA LISHE
      • VIWANDA BIASHARA NA UWEKEZAJI
      • KILIMO MIFUGO NA UVUVI
      • MIPANGO NA URATIBU
      • UTAWALA NA USIMAMIZI WA RASILIMALI WATU
    • Units
      • USIMAMIZI WA TAKA NGUMU NA USAFI WA MAZINGIRA
      • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
      • FEDHA NA UHASIBU
      • HUDUMA ZA SHERIA
      • UKAGUZI WA NDANI
      • USIMAMIZI WA UNUNUZI
      • TEHAMA
      • MAWASILIANO SERIKALINI
      • NMALIASILI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
      • MALIASILI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
  • Investment opportunities
    • Agriculture
    • Livestock
  • Our Services
    • Health
    • Education
    • Agriculture
  • Councillors
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Ratiba
      • Ratiba
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipango Miji Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Uchumi Elimu Afya na Maji
  • Projects
    • Proposed Projects
    • On-going-Projects
    • Completed Projects
  • Publications
    • Brochures
    • By Law
    • Strategic Plan
    • Reports
  • Media Centre
    • Video
    • Press Release
    • Speeches
    • Photo Gallery

Mkurugenzi Simbeye Apongezwa kwa Uongozi Bora kwenye Maadhimisho ya MEOS Day Kasulu TC

Posted on: November 30th, 2025

Katika kilele cha maadhimisho ya MEOS Day, watendaji wa mitaa wa Halmashauri ya Mji wa Kasulu wamemkabidhi cheti cha pongezi Mkurugenzi wa Halmashauri, Mwl. Vumilia J. Simbeye, kama ishara ya kutambua mchango wake mkubwa katika kusimamia kwa weledi utendaji wa watumishi hao na kuiongoza halmashauri kwa ufanisi.

Maadhimisho hayo yaliyofanyika katika maeneo mbalimbali ndani ya mji wa Kasulu yalijumuisha shughuli za kijamii na kiutamaduni, ikiwemo bonanza la michezo mbalimbali lililolenga kuimarisha afya na mshikamano miongoni mwa watendaji. Aidha, watendaji hao walitembelea kituo cha kulelea watoto yatima cha Center of Hope ambapo walikabidhi msaada kwa watoto hao kama sehemu ya kujenga jamii yenye huruma na uwajibikaji.

Katika hafla ya usiku iliyohitimisha maadhimisho hayo, viongozi mbalimbali wa wilaya walihudhuria akiwemo Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Kasulu, Ibrahim Mwangarume, ambaye alikuwa mgeni rasmi kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya. Pia walikuwepo wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama pamoja na viongozi wengine wa serikali.

Akitoa salamu za serikali, Mwangarume aliwataka watendaji wa mitaa kuwa mabalozi wa maadili mema, hasa kwa vijana, akibainisha changamoto ya matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii ambayo imeikumba jamii kwa kasi. Aliwahimiza kuwa viongozi wenye heshima, ustaarabu na mfano bora wa kuigwa katika maeneo yao.

Aidha, aliwasisitiza kuongoza kwa kufuata Dira ya Maendeleo ya Taifa, kuibua miradi bunifu ya maendeleo, na kujiongezea maarifa ili waweze kuwaongoza wananchi kwa uelewa mpana na wa kisasa. Mwangarume alisifu ubunifu wa watendaji hao kuanzisha umoja wao maalum, akiwataka kuendelea kudumisha mshikamano na kuzijengea hamasa halmashauri nyingine kuiga mfano huo.

Katika tukio lilogusa mioyo ya wengi, watendaji wa mitaa walimkabidhi Mkurugenzi Simbeye cheti cha pongezi, wakimuelezea kuwa ni kiongozi mwenye maono, uwajibikaji na anayewajali watumishi wake. Walisema uongozi wake umewawezesha kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi na kuimarisha utendaji katika ngazi za mitaa.

MEOS Day imeendelea kujidhihirisha kama jukwaa muhimu la kuonesha mshikamano wa watendaji wa mitaa na kuibua jitihada za kuboresha utumishi wa umma kwa manufaa ya jamii nzima ya Kasulu

Announcements

  • NAFASI ZA KAZI March 19, 2025
  • TANGAZO LA UBORESHAJI DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA April 30, 2025
  • TANGAZO LA KAZI July 01, 2025
  • View All

Latest News

  • Mkurugenzi Simbeye Apongezwa kwa Uongozi Bora kwenye Maadhimisho ya MEOS Day Kasulu TC

    November 30, 2025
  • Madiwani wapya Kuapishwa Leo

    December 02, 2025
  • Mkurugenzi wa Kasulu Mji Aibua Neema kwa Wapenzi wa Michezo, Azindua Uwanja Mpya wa Volleyball

    November 08, 2025
  • TUDUMISHE UTAMADUNI WA USAFI KILA SIKU : MWANGARUME

    October 25, 2025
  • View All

Video

UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA
More Videos

Quick Links

  • News

Related Links

  • TAMISEMI
  • Ega
  • Utumishi
  • Kigoma Region

World visitors tracker

world map hits counter

Contact Us

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service
    • Test

Copyright ©2017 Kasulu Town Council. All rights reserved.