• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Kasulu Town Council
Kasulu Town Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Kasulu Town Council

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Strategies
  • Administration
    • Organisation Structure
    • Department
      • ELIMU SEKONDARI
      • ELIMU AWALI NA MSINGI
        • MAENDELEO YA JAMII
      • MAENDELEO YA JAMII
      • MIUNDOMBINU MAENDELEO YA MJINI NA VIJIJINI
      • HUDUMA ZA AFYA USTAWI WA JAMII NA LISHE
      • VIWANDA BIASHARA NA UWEKEZAJI
      • KILIMO MIFUGO NA UVUVI
      • MIPANGO NA URATIBU
      • UTAWALA NA USIMAMIZI WA RASILIMALI WATU
    • Units
      • USIMAMIZI WA TAKA NGUMU NA USAFI WA MAZINGIRA
      • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
      • FEDHA NA UHASIBU
      • HUDUMA ZA SHERIA
      • UKAGUZI WA NDANI
      • USIMAMIZI WA UNUNUZI
      • TEHAMA
      • MAWASILIANO SERIKALINI
      • NMALIASILI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
      • MALIASILI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
  • Investment opportunities
    • Agriculture
    • Livestock
  • Our Services
    • Health
    • Education
    • Agriculture
  • Councillors
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Ratiba
      • Ratiba
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipango Miji Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Uchumi Elimu Afya na Maji
  • Projects
    • Proposed Projects
    • On-going-Projects
    • Completed Projects
  • Publications
    • Brochures
    • By Law
    • Strategic Plan
    • Reports
  • Media Centre
    • Video
    • Press Release
    • Speeches
    • Photo Gallery

WANANCHI WAJITOKEZA KWA WINGI KIJIANDIKISHA KUPIGA KURA,WAVUKA MALENGO

Posted on: October 20th, 2024

Wananchi wa Halmashauri ya Mji wa Kasulu Mkoani Kigoma wamejitokeza kwa wingi kujiandikisha ili kupiga kura siku ya Jumatano tarehe 27/11/2024.

Akitoa taarifa ya zoezi hili la uandikishaji wa wapiga kura; Msimamizi wa Uchaguzi Mwalimu Vumila Julius Simbeye amesema zoezi la uandikishaji wa wapiga kura  lilianza tarehe 11/10/2024 na kukamilika tarehe 20/10/2024 na kuchukua jumla ya siku  kumi (10). Zoezi la Uandikishaji limefanyika katika Kata kumi na tano (15) zenye Tarafa mbili za Heru chini na Heru juu na kujumuisha vituo miamoja kumi na saba (117) vya kujiandisha kupiga kura.

Aidha, jumla ya wapiga kura Mia moja ishirini na tatu elfu miambili hamsini na nne (123,254) wamejiandikisha wakiwemo wanaume (ME) Hamsini na saba elfu  miambili sabini na tano (57,275) wanawake (KE) sitini na tano elfu mia tisa sabini na tisa (65,979 )  sawa   asilimia 101    Malengo yalikuwa ni kuandikisha wapiga kura Mia moja ishirini na mbili elfu na arobaini na mbili  (122,042). 

Vituo vya uandikishaji wa wapiga kura vilifunguliwa saa mbili kamili asubuhi na kufungwa saa kumi na mbili kamili jioni.

Uandikishaji huu umefanyika ili wananchi wa Halmashauri ya Mji wa Kasulu waweze kupata fursa ya kumchagua Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa na Wajumbe wake; kadiri ya Mwongozo wa Uchaguzi wa viongozi ngazi za Vijiji, Vitongoji na Mitaa uliotolewa Agosti, 2024 unavyoelekeza.

Orodha ya wapigakura itabandikwa leo tarehe 21/10/2024 kwenye mbao za matangazo na msimamizi wa uchaguzi ili kuwezezesha wananchi kukagua wapiga kura kwa ajili ya usahihi wa orodha hiyo, Kurekebisha jina la mpiga kura, kubadilisha taarifa iliyopo kwenye orodha hiyo na kufuta jina lililo orodheshwa kwa vile aliyeorodheshwa  amekosa sifa za mpiga kura, zoezi la ukaguzi wa orodha ya wapiga kura litaendelea mpaka tarehe 27/10/2024 siku ya Jumatano.

Msimamizi wa Uchaguzi, Mwalimu Simbeye anawashukuru wananchi wa Halmashauri ya Mji wa Kasulu kwa kujitokeza kwa wingi na kujiandisha ili waweze kupiga kura, amewasihi pia kujitokeza kwa wingi siku ya uchaguzi tarehe 27/11/2024 ili kuwachagua viongozi wao watakaowaongoza kwa kipindi cha miaka mitano, Aidha anawashukuru kwa utulivu uliokuwepo kwa kipindi chote cha uadikishaji wa wapiga kura. Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Kigoma, Mungu ibariki Halmashauri ya Mji Kasulu.

Announcements

  • NAFASI ZA KAZI March 19, 2025
  • TANGAZO LA UBORESHAJI DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA April 30, 2025
  • View All

Latest News

  • KAIMU KATIBU TAWALA MKOA NDUGU ELIASANTE M.MBOELO AKABIDHIWA VIFAA TIBA HUDUMA ZA MACHO MKOANI KIGOMA

    May 08, 2025
  • KAIMU KATIBU TAWALA MKOA NDUGU ELIASANTE M.MBOELO AKABIDHIWA VIFAA TIBA HUDUMA ZA MACHO MKOANI KIGOMA

    May 08, 2025
  • KAIMU KATIBU TAWALA MKOA NDUGU ELIASANTE M.MBOELO AKABIDHIWA VIFAA TIBA HUDUMA ZA MACHO MKOANI KIGOMA

    May 08, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI KASULU TC LATOA PONGEZI

    May 05, 2025
  • View All

Video

UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA
More Videos

Quick Links

  • News

Related Links

  • TAMISEMI
  • Ega
  • Utumishi
  • Kigoma Region

World visitors tracker

world map hits counter

Contact Us

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service
    • Test

Copyright ©2017 Kasulu Town Council. All rights reserved.